• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ni Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Dkt. Mwingulu Nchemba akiwaeleza wananchi maamuzi ya viongozi baada ya kuusikiliza mgogoro uliodaiwa kuwepo kati ya Wananchi na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika kiji

Posted on: November 14th, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@2020.go.tz

Singida - Iramba. Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ni Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Dkt. Mwingulu Nchemba amesikiliza wananchi na kutatua mgororo unaodaiwa kuibuka punde baada ya Wakala wa Huduma za  Misitu Tanzania (TFS) kuweka mabango ya matangazo yanayokataza shughuli za kilimo,mifugo na alama za mipaka katika eneo hilo.

Dkt Nchemba ametatua mgogoro huo leo Jumamosi Novemba 13, 2021 wakati akiongea na wananchi wa kijiji cha Mpambaa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba mkoa wa Singida.

Aliwafahamisha wananchi hao kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, Suleiman Mwenda ameridhia kuwa eneo hilo ambalo wanalima na kuishi waendelee na huku ambako hakulimwi kubakie kuwa ni eneo la malisho ya mifugo na kupanda miti inayosimamiwa na Wakala wa Huduma wa Misitu Tanzania (TFS).

“Ni lazima ndugu zangu mlime kwa sababu kilimo ni uhai wa mwanadamu, hivyo serikali ya kijiji mjipange ili muhakikishe watu wote wanapata sehemu ya kulima” alisema Waziri Nchemba na kuongeza kuwa

“Hatuwezi kuuwa mradi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na pia hatuwezi kuuwa shughuli za ufugaji, hivyo upande waliopo wananchi utaendelea na shughuli za mifugo na kilimo huku shughuli za TFS zikiendelea upande wa pili kwa kupanda miti ambayo inamanufaa katika maisha yetu.”

Dtk Nchemba aliwaomba wananchi na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kuligawa eneo hilo lenye ukubwa wa takribani hekari 9651 linalodaiwa kuibuwa mgogoro kuwa nusu liwe la kilimo na makazi huku lile la TFS litumike kwa ajili ya kupanda miti pamoja na malisho ya mifugo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda aliwahakikishia wananchi hao kuwa kila mmoja atapata eneo la kulima.

“Niwahakikishie kila mmoja atapata shamba la kulima na asijitokeze yoyote akadai kuwa eneo hili ni mali yake, ardhi hii kwa sasa itabaki kuwa ni mali ya kijiji mpaka pale tutakapokuja kuigawa kwa wananchi wote.” Alisisitiza Mwenda

Kwa upande wake Mhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wilayani hapa, Shabani Nyamasangara aliwaomba wananchi hao wasitoe mabango hayo pamoja na alama za mipaka wakati wakiwa wanaandaa utaratibu wa kuja kuyatoa.

Akiongea na mwandishi wetu, mmoja wa wananchi waliofika katika utatuzi wa mgogoro huo, Mathius  Imambo, amewataka wananchi wenzake kuridhika na maamuzi yaliotolewa, huku akiwasihi kudumisha amani, kuzingatia taratibu na sheria ili kujiepusha na migogoro isiyokuwa na tija katika kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Naye Anastazia Kitundu akamshukuru Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Mwigulu Nchemba pamoja na Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kuupatia ufumbuzi mgogoro huo.

“Niwashukuru sana kwa sababu tulikuwa hatuna pakukimbilia wakati tunawatoto na vikongwe tunaoishi nao hapa, Kwakweli Mungu awasaidie na kuwabariki sana katika maisha yenu ili mlitumikie Taifa hili kwa muda mrefu.” alishukuru Kitundu

Mgogoro uliotatuliwa ulidaiwa kuibuka baada ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kuweka mabango yenye matangazo yanayokataza kuchoma moto misitu, kukata miti ovyo, kuhamisha mpaka wa msitu, kuingiza mifugo msituni, kutengeneza mkaa na kulima kwenye eneo la hifadhi.

Mwisho

Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ni Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Dkt. Mwingulu Nchemba akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda kushoto wakitembelea eneo lililodaiwa kuibuwa mgogoro kati ya Wananchi na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika kijiji cha Mpambaa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Waziri wa Fedha na Mipango ambaye ni Mbunge wa jimbo la Iramba Magharibi, Dkt. Mwingulu Nchemba akiwataka wananchi kumshukuru Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda kwa namna ambavyo amejitahidi kuusikiliza mgogoro uliodaiwa kuwepo kati ya Wananchi na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika kijiji cha Mpambaa Tarafa ya Shelui wilayani Iramba mkoa wa Singida. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.