• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Harison Mwakyembe amewafunda waandishi wa habari Mkoani Singida

Posted on: January 22nd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba.Waziri wa Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Harison Mwakyembe amekemea tabia ya baadhi ya waandishi wa habari kufanya usaili(interview) na viongozi mbalimbali baada ya hutuba zao.

Waziri huyo ameyasema hayo leo Ijamatano Januari 22, 2020 wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari  katika kikao  na Waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida  kilichofanyika katika  ukumbi wa ofisi ya Madini mjini hapa.

Dkt, Mwakyembe amesema kuwa kufanya usaili baada ya hotuba ya kiongozi ni uzembe, uvivu na upotoshaji wa habari husika kwani kiongozi alikwisha zungumza katika hutuba yake hivyo si busara kufanyiwa usali tena.

Amesema kuwa kuna baadhi ya waandishi wa habari wakilalimika kuhusu kutokuwa na uhuru wa kupata habari  ambapo alinukuu kipengele cha Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ibara ya 18 kifungu kidogo (d) ambacho kinasema

“kila mtu ana uhuru wa kupata taarifa wakati wowote”

Amesema wataalam wanaiona ibara hiyo kuwa ndio msingi wa kidemokrasia kutimiza haki ya wananchi kupata taarifa zilizokuwa sahihi.

“Ni wazi kuwa duniani kote tasnia ya habari haijaacha sekta binafsi kuwa na tafsiri ya uhuru wa habari usiokuwa na mipaka.

Aidha Waziri huyo ametolea mfano wa wakongwe wa habari kama Uingereza wa shirika lao la habari (BBC)  kutangaza kwa lugha 40 ili kulinda dhima ya Taifa kimila na desturi.

“ Mwananchi  anapaswa kupewa taarifa yenye kukidhi vigezo vyote vya taarifa sahihi,”alisisitiza na kuongeza Dkt, Mwakyembe

“Waandishi wa habari mnatakiwa kuyaeleza mazuri yanayofanywa na serikali ikiwa  pamoja na Tanzania kuwa nchi ya kwanza kuingia kwenye teknolojia ya analogi na kwenda kwenye teknolojia ya  digitali, hii imepelekea Tanzania kusifika  katika taaluma ya mambo ya habari  Barani Afrika  ikifuatiwa na nchi ya Rwanda”

Pia kutimiza maslahi mapana ya wananchi kupata habari bila malipo na kulida tunu ya Taifa kwa kuzingatia maadili na desturi ya tasnia ya habari.

Aidha amewataka waandishi hao  kufahamu sheria ya kupata habari (Access to information Act ) na ile ya Huduma ya vyombo vya habari (Media service Act ya 2016) ili kupata vigezo vya kua na weledi na maadili ya taaluma hiyo.

Amesema kufuatia sheria ya kupata habari, waandishi wa habari wametakiwa kufahamu kuwa kila taasisi inamsemaji wake mkuu hivyo inawapasa kuchukua  taarifa sahihi na za uhakika kutoka kwa wasemaji hao  huku wakilinda uhuru wa habari na  kulinda maslahi, maadili  ya nchi na  usalama wake.

Kwa mujibu wa  sheria ya huduma ya vyombo vya habari inawataka waandishi wa habari kuwa na weledi wa ngazi ya stashahada, digrii na kuendelea, ambaye atakosa sifa hizo, hatokuwa na sifa ya kuwa mwandishi wa  habari.

Hata hivyo waandishi wa habari wametakiwa kuielewa nia ya serikali kuleta sheria hiyo ni kutaka kuwa na wanahabari wenye weledi na ujuzi mpana wa tasnia hiyo.

Vile vile Dkt. Mwakyembe  ameahidi kufuatilia uwepo wa mtaala mmoja utakaotumika kwenye vyuo vyote vinavyotoa tasnia hiyo nchi nzima.

Akiwasilisha kero na changamoto za waandishi wa habari wa mkoa huo Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Singida  Seif Takaza amemuhakikishia Waziri Dkt, Mwakyembe kuwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida wanafanya kazi kwa waledi mkubwa ingawa 99% ni waandishi wakujitegemea.

Waandishi  hao wana changamoto yakutokuwa na mikataba ya kazi, kutolipwa vizuri na kwa wakati hali ambayo imesababisha kushindwa kujiendeleza kielimu kutekeleza matakwa ya sheria husika.

“Mhe, Waziri tunaishukuru serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na kuteuliwa kwako  wewe kuwaWaziri wa tasnia hii ambayo imeshika kasi ya maendeleo, bila vyombo vya habari wananchi wasinge yaona maendeleo na sifa kemu kemu anazopata Rais wetu kupitia vyombo hivi, hivyo tunaomba serikali kupitia Wizara yako kuwasaidia wanahabari wanaotaka kujiendeleza kielimu ili kukidhi matakwa ya serikali ya kila mwandishi wa habari kuwa na kiwango cha elimu ya stashahada kwani waandishi wengi kipato chao hakikidhi kujisomesha wenyewe kwa kiwango wanachopata katika vyombo vyao wanavyovitumikia” amesema Takaza

Pia Mwenyekiti huyo ameiomba serikali kuzitambuwa klabu za waandishi wa habari kuwa taasisi muhimu kama zilivyo taasisi zingine, hivyo ameiomba serikali  iwape  maeneo ya kujenga ofisi za klabu  ili kuepukana na kupanga nyumba za watu binafsi, kwani changamoto hii ni ya  klabu za nchi nzima .

Halikadhalika Mwenyekiti huyo ameishukuru serikali kwa kuwaandalia mpango mzuri wa bima ya afya kwa waandishi wote ambao ni wanachama wa klabu za waandishi wa habari.

 

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Habari Maelezo, Rodney Thadeus amewakumbusha waandishi wa habari umuhimu wa kuwa na kitambulisho (Press Card), kinachomtambulisha mwandishi wa habari na kuhifadhiwa kwenye kanzi data ya Habari Maelezo.

Pia ni rahisi kwa Mwandishi huyo anapokutwa na tatizo kusaidiwa kwa haraka na kutokusigana  wakati anapotekeleza majukumu yake.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA November 03, 2023
  • KUITWA KAZINI November 29, 2023
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2018 HALMASHAURI YA WILAYA IRAMBA January 05, 2019
  • MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2018 January 05, 2019
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wamefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa Wilayani Iramba

    October 24, 2023
  • RAIS DKT. SAMIA AHITIMISHA ZIARA YAKE MKOANI SINGIDA KWA KISHINDO, WANANCHI WAMSHUKURU KWA MIRADI YA MAENDELEO

    October 17, 2023
  • MKUU wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba amepokea rasmi Mbio za Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoani Tabora na aliyekabidhi ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Balozi Batlida Briani.

    September 22, 2023
  • MKIMBIZA Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Abdalla Shaibu Kaim amewataka Watanzania kuhakikisha wanakemea vitendo vya rushwa kwa maelezo kuwa rushwa inakwamisha maendeleo ya Mkoa pamoja na Taifa kwa ujumla

    September 22, 2023
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.