• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba ahidi kutoa kompyuta kwa shule za Iramba zilizoingia kumi bora kimkoa Singida.

Posted on: June 3rd, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

tehama@irambadc.go.tz

Iramba. Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Mwigulu Nchemba ameahidi kuzipa kopyuta mpya za kisasa shule nne za Kata za Wilayani Iramba zilizofanya vizuri katika matokeo ya mwaka 2019 ikiwa ni motisha ya kuongeza ufaulu Wilayani humo.

Waziri huyo ametoa ahadi hiyo leo Jumanne 02, 2020 wakati akitoa salamu zake katika Baraza la Madiwani wa Halamshauri hiyo Ukumbi Mkubwa Mjini Kiomboi.

“Nitawapatia kompyuta mpya za kisasa hizo shule ili kuweza kusaidia taratibu hizi za kisasa za uandaaji wa masomo ya wanafunzi,” amesema Waziri Nchemba

Lengo likiwa ni kuwachochea Walimu kwa kazi nzuri wanazo zifanya chini ya usimamizi mzuri wa Mkuu wa Wilaya yetu, Emmanuel Luhahula.

Pia, amewaomba Madiwani kuwahamasisha watoto pindi shule zitakapofunguliwa kuwapa nafasi Walimu ambao wamefika Wilayani hapo kwa ajili ya kufundisha lugha mbalimbali za kitaifa na Kimataifa.

“Lugha ni ajira na wanaweza kupata soko kwa nchi ambazo zitakazohitaji mtu ambaye anajua lugha yao na Kiswahili kwakuwa Rais amekwisha kitangaza sana Kiswahili Kimataifa,” amesema Nchemba na kuongeza

“Yule atakaejua Kifaransa anaweza kupata ajira ukanda wakati, Kiarabu kwa ukanda wa kiarabu na Kireno kwa ukanda mwinge,”

“Pia, Taifa linahitaji wafanyabiashara wazalendo wakiwa wanaweza hizo lugha,watakua na uwezo wa kumudu biashara mbalimbali duniani.”

Akifafanua kuhusu ufaulu wa wanafunzi matokeo ya mwaka jana, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri hiyo, Godfrey Mwanjala amesema kuwa kompyuta hizo zitatolewa kwa shule ambazo zimekua zina vifaa hivyo vichache.

Mwanjala amezitaja shule hizo kuwa ni Kyengege Sekondari, Kisana Sekondari, Mgongo Sekondari na Kidaru ambazo zimeingia kumi bora kimkoa Singida.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya hiyo, Emmanuel Luhahula amewasifu Madiwani hao kwa kukubali na kulinda msitu wa Sekenge Tulya kuwa hifadhi.

Aidha ameonesha masikitiko yake kwa Watendaji kwa kuwa msitu huo unaendelea kuisha pamoja nakuwa ulipitishwa kuwa hifadhi.

“Watendaji wenzangu wa Serikali nendeni mkasimamie misitu hiyo kwa kuwa imekwishapitishwa kuwa ni hifadhi maana watu wanavuna misitu kama vile haina wenyewe,” amesikitika Luhahula

Halikadhalika, ameonesha imani yake kwa viongozi hao kuwa makini namna wanavyoshughulikia hoja na kuhakikisha Halmashauri hiyo inapata hati safi kwa miaka 5 mfululizo, hivyo kuacha historia ambayo haikuwako miaka michache iliyopita.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Wilayani humo, Ashery Joel amewaomba madiwani hao kuliangalia sana suala la usambazaji wa umeme warea vijijini.

“Ninaomba Mkurugenzi na Madiwani kuendelea kufuatilia usambazaji wa umeme warea  kwa kua kuna baadhi ya maeneo baadhi ya kaya zimepata na baadhi hazijapata, hivyo hizo ni kero kwa mtu ambaye hajapata umeme kwati tumeambiwa kila mtu ataupata umeme,” amesema Joel

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akifafanua jambo wakati alipokua akiongea na Madiwani pamoja na Watumishi mbalimbali Ukumbi Mkubwa wa Halmashuri hiyo mjini Kiomboi. Picha na Hemedi Munga

    Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Ashery Joel  akiwaasa Madiwani kuhakikisha wanamaliza kipindi chao vizuri. Picha na Hemedi Munga

Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakifuatilia hoja mbalimbali Ukumbi Mkubwa wa Halmashauri hiyo. Picha na Hemedi Munga


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.