• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kutokuwa na madeni ya wakulima wa zao la pamba msimu wa 2018/2019 na 2019/2020.

Posted on: August 10th, 2020

Hemedi Munga, Irambadc

ded.irambadc@singida.go.tz

Iramba. Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Iramba kwa kutokuwa na madeni yatokanayo na zao la pamba toka kwa wakulima  walioko katika AMCOs ya Malendi na Shelui.

Waziri Hasunga ametoa pogenzi hizo leo agosti 10, 2020 wakati alipofanya ziara katika AMCOs ya Malendi na Shelui Wilayani hapa.

“ Nimefurahi sana kwa kuwa leo nimekuja kukagua pamba inayozalishwa na madeni kama wapo wanaodai hawajalipwa mwaka jana na kwa kuwa nyie hamna anaye dai ninawapongeza sana” amepongeza na kuongeza kuwa

“Ni wakati sasa wakulima wa pamba kuhakikisha wanalima pamba kisasa kwa kutumia mbegu bora ili waweze kupata kilo 1500 kwa hekari moja, hivyo mkulima ataona faida ya kilimo.”

Amefafanua kuwa mkulima atakapopata pamba yake Serikali haitaki kusikia mwanchi hajalipwa fedha zake, kila aliye lima pamba alipwe fedha zake kwa wakati ili nao wafurahie maisha.

“Ninaomba niwaambie Wakulima wenzangu kuwa pamba hii ndio inatuletea fedha za kigeni, ikachakatwe tuweze kupata nguo tunazo vaa, hivyo pamba ni zao la mkakati wa kitaifa ambayo tunataka kuhakikisha inalimwa na kwa ufanisi ili mkulima apate mavuno bora.” amesema Waziri

Amefafanua kuwa kilimo ndio maisha yetu kwa sababu kinatupatia chakula, fedha, kinatoa malighafi, kinatoa ajira na kinajenga uchumi.

“Limeni kwa wingi ili mle maisha maana hata vitabu vya dini vinasema na asiye fanya kazi na asile, hivyo kila mmoja lazima afanye kazi ikiwemo kilimo, ufugaji na uvuvi pindi inapowezekana.” amesisitiza Waziri

Akitoa taarifa fupi mbele ya Waziri huyo, Afisa Kilimo wa Halmashauri hiyo, Marietha Kasongo amesema kuwa Wilaya ya Iramba inalima mazao ya chakula ambayo ni mahindi, mpunga, mtama, uwele,viazi vitamu, muhogo, maharage na kunde, huku zao la  alizeti, pamba, vitunguu, karanga na dengu kuwa zao la biashara.

Marietha amesema kuwa Iramba haitakuwa na njaa kwa sababu msimu wa kilimo 2018/2019 ilizalisha tani 154,791 ya mazao ya chakula na ziada ni tani 87,714 huku msimu wa 2019/2020 ilizalisha tani 224,334 na kuwa na ziada 156,847 na kufanya hali cha kula kuwa nzuri katika wilaya yetu.

Akiongea kuhusu kilimo cha pamba, Kasongo amesema kuwa kilimo hicho kinaendelea kuimarika kwa kuwa wakulima wanakipenda.

“Kupitia AMCOs imeweza kukusanya takribani Kg 2, 040, 490 zenye thamani ya takriban Tsh 2.4milioni kwa misimu wa 2018/2019 huku msimu wa 2019/2020 imekusanya Kg 5milioni” amebainisha Kasongo

Halikadhalika, ameishukuru kampuni ya Biosustaini kwa kununua pamba kwa Tsh 900 kwa kilo ambapo takribani Kg 134,920 zenye thamani ya takribani 121.4milioni zimelipwa.

Kwa upande wake mmoja wa wanachama wa AMCOs hiyo, Rubeni Kabila ametoa kero yake kwa Waziri huyo, kuwa kuna dawa wanazo nunua lakina zinashindwa kuua vidudu waliopo katika mmea wa pamba.

“Tunashindwa kunufaika na kilimo cha kisasa kutokana na uwepo wa kiua dudu licha yakuwa tunajitahidi kulima kitaalam pamoja na kutunza shamba vizuri lakini wadudu wanashambulia, hivyo tunaiomba Serikali kutusaidia kupata dawa inayofaa kuua vidudu.” ameomba kabila

Naye katibu wa AMCOs hiyo, Magulya Malendela amesema kuwa kupitia AMCOs ya Malendi wameweza kuchangia mifuko mitano ya simenti kwenye ujenzi wa zahanati ya kijiji na michango mingine kwenye sekondari ya Mgongo.

MWISHO

Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula akimuonesha Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga zao la pamba wakati alipotembelea AMCOs ya malendi agosti 10, 2020. Picha na Hemedi Munga

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Linno Mwageni akisalimiana na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga wakati alipotembelea AMCOs ya Malendi agosti 10, 2020. Picha na Hemedi Munga

Afisa Kilimo na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Marietha Kasongo akisalimiana na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga wakati alipotembelea AMCOs ya Malendi agosti 10, 2020. Picha na Hemedi Munga

Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga akikagua pamba iliyokusanywa na AMCOs ya Malendi wakati alipofanya ziara katika kijiji hicho agosti 10, 2020. Picha na Hemedi Munga

Afisa Kilimo na Ushirika, Marietha Kasongo kushoto na Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula kulia wakimuongoza Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga kukagua zao la pamba katika AMCOs zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Iramba wakati alipofanya ziara agosti 10, 2020.Picha na Hemedi Munga

Zao la pamba AMCOs ya Malendi ikiwa tayari kwa ajili ya kuuzwa. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.