• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe, January Makamba amefanya Ziara ya kutembelea Ziwa Kitangiri na Bwawa la Ushora Wilayani Iramba mkoa wa Singida.

Posted on: August 21st, 2018

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mheshimiwa January Makamba, ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe. Emmanuel Luhahula, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashari ya Wilaya ya Iramba Mwl.Linno Mwageni, Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Iramba na Wakuu wa Idara na Vitengo wamefanya ziara ya kukagua baadhi ya maeneo yanayohusisha miradi ya mazingira Wiliyani Iramba mkoa wa Singida.

Mheshimiwa Makamba katika ziara yake Wilayani Iramba aliweza kudhuru katika maeneo ya Bwawa la Ushora lililopo Kata ya Urughu Tarafa ya Ndago pamoja na Kutembelea Ziwa la Kitangiri katika Kata ya Tulya, Tarafa ya Shelui wilaya ya Iramba.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mhe, Simion Tiyosera Diwani wa kata ya Urughu(CCM), akiongea kwa niamba ya wananchi wa Iramba ameomba Waziri Makamba kurejea mpaka wa kimahesabu kati ya ramani ya Mkoa wa Singida na Iliyokuwa Shinyanga. Hii itasaidia mmiliki wa rasilimali ya Ziwa ambaye ni Halmashauri ya wilaya ya Iramba na kutoa mwongozo shirikishi wa kutunza na kuendeleza rasilimali ya Ziwa kwa manufaa ya watanzania wote na Wizara kusaidia Mpango wa Hifadhi ya Ziwa Kitangiri, na Bwawa la Ushora kwa ajili ya manufaa ya watanzania wa kizazi cha sasa na kinachokuja.

Mhe, Tiyosera aliongeza kusema, Ziwa Kitangiri lina ukubwa wa eneo la kilomita za mraba 105, takwimu za kisayansi na watafiti mbalimbali zinaonyesha kina cha maji kimepungua toka mita tisa (9) hadi chini ya mita sita (6) na kupungua kwa ukubwa wa Ziwa kwa zaidi ya 38% katika kipindi cha kuanzia mwaka 1972 hadi 2016.

Waziri Makamba amesisitiza Utashi, Utayari na Uwezo, Utunzaji mazingira na utunzaji wa Vyanzo vya Maji na Misitu katika maeneo ya jamii. “Maeneo ambayo tunaamua kuyaifadhi ni maeneo ambayo wananchi wenyewe wameamua tuyaifadhi. Tunapokubaliana eneo liifadhiwe, basi lazima kuwe na Utashi wa wananchi wenyewe, utayari na uwezo wao wa kuhakikisha wanalinda maeneo hayo na yanakuwa salama.”

Mhe. Makamba alisema kwamba Uhifadhi wa mazingira unahitaji wananchi wawetayari kujitoa na kuwa walinzi wao wenyewe na kushauriana na Serikali kwenda nao bega kwa bega kuhakikisha wanasaidiana katika utunzaji wa rasilimali hizo.

Ziwa kitangiri ni moja ya rasilimali muhimu, iliyopo katika Wilaya ya Iramba, ambalo linapakana na Wilaya ya Meatu kwa upande wa Mkoa wa Simiyu, kishapu upande wa Mkoa wa Shinyanga na Igunga kwa upande wa Tabora. Shughuli mbalimbali za uvuvi zinazofanyika katika Ziwa hili zimekuwa zikitoa mchango mkubwa katika kuboresha lishe ya jamii na kukuza uchumi wa kipato cha kaya, kuboresha maisha na maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla na hatimaye kufikia kiwango cha uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.


Waziri Januari Makamba akisalimiana na wananchi wa Kata ya Urughu.

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.