• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu ameahidi kujenga daraja mto Kinshoka Wilayani Iramba Mkoa wa Singida

Posted on: December 23rd, 2021

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

Singida - Iramba. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Ummy Mwalimu amewaahidi wakazi wa kijiji cha Tintigulu kujenga daraja mto Kinshoka ili kupunguza adha ya kupata huduma za afya pindi mvua zinapokuwa zinanyesha na kusababisha kukatika kwa mawasiliano kwa baadhi ya nyakati.

Waziri Ummy ametoa ahadi wakati alipofanya ziara ya  kufungua ujenzi wa barabara yenye kilometa 7.3 kutoka Shelui mpaka kijiji cha Tintigulu wilayani Iramba Mkoa wa Singida.

“Ndugu zangu ingependeza sana kama tungeanza kujenga daraja kisha ujenzi wa barabara ukafuata.” Amesema waziri huyo na kuongeza kuwa

“Mhe, Rais amedhamiria kufungua barabara za vijijini na mijini ndio sababu kwa Wilaya ya Iramba imetengewa Tsh 7.3 bilioni kwa mwaka wa fedha ukilinganisha na bajeti ya mwaka jana ambapo ilitengewa takribani milioni mia nane (800,000,000). Hivyo kipaombele cha daraja ni muhimu sana.”

Akiwasilisha taarifa fupi kwa Waziri huyo Meneja wa TARURA Wilayani hapo, Mhandisi Evance Kibona amesema kuwa ujenzi huo utahusisha kusafisha eneo la barabara ukubwa wa hekta 8.78, kutengeneza tuta la barabara kilometa 7.3, kuweka changarawe kwa ujazo wa eneo ( ) 7665, kujenga karavati lenye milango 3 yenye upana wa mita 4.5 kilometa 3, kujenga makaravati 14 yenye upana wa mita 2 kilometa 1.5 na kujenga kivuko (drift) chenye ukubwa wa mita 27 kwa mita 5.

Amebainisha kuwa kumalizika kwa barabara hii kutasaidia kufungua mawasiliano na shughuli za uchumi katika vijiji 6 vilivyopo kati ya kata ya Shelui na Ntwike vyenye jumla ya wakazi 14,933 wilayani hapo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Tintigulu Wilayani hapo, Nkeno Nkamba amemshuku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa sababu amewaletea fedha za kutengeneza barabara hiyo, wakiamini kuwa barabara hiyo itawasaidia kupita kwa urahisi kuja kituo cha afya kilichopo Shelui ambapo ni takribani kilometa 7.3.

Naye Elipendo Jumanne mkazi wa kijiji cha Tintigulu ameiomba serikali kuikamilisha barabara hiyo kwa haraka ili iwe rahisi kupata huduma za afya hasa wakati wa kujifungua.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • KIDATO CHA KWANZA KURIPOTI SHULE January 13, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • MAAFISA ELIMU KATA 136 MKOANI SINGIDA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHULE NA UJAZAJI TAKWIMU KATIKA MFUMO WA "SIS"

    March 24, 2025
  • DC MWENDA AWASISITIZA WALIPA KODI KUFANYA MAKADIRIO YA KODI KABLA YA MACHI 31, 2025

    March 20, 2025
  • DC MWENDA NA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA WACHANGIA JUMLA YA MADAWATI 98 SHULE YA MSINGI MSANSAO ILIYOPO KATA YA MTEKENTE

    March 10, 2025
  • WALIMU WAKUU 108 WA SHULE ZA MSINGI NA MAAFISA ELIMU KATA 20 WILAYANI IRAMBA WAPEWA MAFUNZO ENDELEVU YA USIMAMIZI WA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI FANISI KUPITIA JUMUIYA ZA KUJIFUNZA ZA WALIMU WAKUU NA MAAFISA ELIMU KATA

    March 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.