• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Wilaya ya Iramba Mkoani Singida imezindua kampeni ya chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi.

Posted on: April 27th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Mhe:Emmanuel Luhahula akiambatana na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwageni leo wamezindua zoezi la utoaji wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi (HPV) ambayo inatolewa kwa Wasichana waliotimiza umri wa Miaka 14. Mkuu wa Wilaya ya Iramba amesema zoezi hilo limeanza leo April 27, 2018. 

 

Vile vile wamezidua mpango wa chanjo ya polio kwa njia ya sindano (IPV) utoaji wa chanjo ya sindano ya kuzuia ugonjwa wa polio kwa watoto wenye umri wa wiki 14.

Chanjo hii inaanza kutolewa kwa njia ya matone mtoto anapozaliwa, anapofikisha wiki 6, wiki 10 nawiki 14. 

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Iramba amesema utoaji wa chanjo hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kukabiliana na ugonjwa wa saratani ambao umekuwa ukisababisha vifo vya kinamama wengi  huku akiitaka jamii kuwa na utamaduni wa kupima afya mara kwa mara.

Pamoja na hayo Mkuu wa Wilaya ya Iramba ametoa wito kwa viongozi wa dini, madiwani, wenyeviti wa Vijiji na wajumbe wa kikao kuhamasisha jamii kuwapeleka watoto wao zahanati au hospitali kupata chanjo hiyo. Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Iramba amesema chanzo cha ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na mapenzi katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi, kuzaa watoto wengi pamoja na uvutajiwa sigara ambapo dalili zake ni kutokwa na damu bila mpangilio, maumivu ya mgongo, miguu, kiuno, kutokwa na uchafu ukeni pamoja na kuchoka, kupungua uzito na hamu ya kula. 

 Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Dkt.Boniface Marwa ametoa Ufafanuzi akisema Saratani ya mlango wa kizazi inasababishwa na virusi vya Human Papilloma ambapo tiba yake kwa hatua ya mwanzo ni kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kubaini dalili za mwanzo na kupata matibabu stahiki.

Vilevle amesema Saratani ya mlango wa kizazi ni saratani ambayo hutokea kwenye via vya uzazi wa mwanamke ambayo ni kiingilio kutoka uke hadi katika mfuko wa uzazi. nimoja kati ya zaidi ya aina 40 ya virusi vya human papilloma (HPV), ambavyo 13 vinasababisha saratani.

Matibabu kwa wagonjwa walio na virusi hivyo yanategemea na viwango vya virusi hivyo mwilini, hata hivyo yanaweza hitaji kutibiwa kwa njia ya upasuaji na kutoa sehemu au mfuko wa uzazi mzima au kutumia miyonzi.


Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.