• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Zaidi ya bilioni 232 zatekeleza miradi ya maendeleo Mkoani Singida

Posted on: April 13th, 2022

Na Hemedi Munga

tehama@irambadc.go.tz

        

Singida - Iramba. Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge amewaagiza Wahandisi wote kuwasimamia kikamilifu mafundi ujenzi ili waongeze nguvu za vibarua hatimaye wakamilishe ujenzi wa miradi ya maendeleo kwa wakati.

Dkt. Mahenge ametoa agizo hilo leo Jumatatu Aprili 12, 2022 wakati alipokuwa akikagua ujenzi wa jengo la Dharura na ICU katika Hospitali ya Kiomboi wilayani Iramba mkoa wa Singida.

“Tunataka jengo lote lionekane kuna watu wanafanya kazi, hivyo msimamizi anayesimamia ujenzi huu aongeze nguvu nakutoa fedha kwa vibarua hao.” Alisema Mkuu huyo wa Mkoa

Aidha, aliongeza kuwa ni lazima tusimamie fedha hizi vizuri ili matunda yaliokusudiwa yafikiwe kwa sababu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amezitafuta fedha hizi ziwanufaishe watanzania.

Katika hatua nyingine, Dkt. Mahenge alimshukuru Rais Samia kwa kuleta fedha zaidi ya Tshs 232 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Singida ikiwemo ujenzi wa shule mpya, madarasa mapya, zahanati, vituo vya afya,ICU, maji na barabara.

Pia, alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda kwa namna alivyoshirikiana na watumishi wote wa wilaya hiyo kusimamia miradi ya maendeleo.

“Ninawapongeza watumishi wote wa wilaya ya Iramba kwa sababu miradi hii inakwenda vizuri.” alipongeza na kuoneza kuwa

“Ni wajibu wetu kusimamia na kufanya ukaguzi wa miradi hii kwa sababu ni fedha nyingi zimeleekezwa katika miradi hii mikubwa, hivyo ni lazima tuisaidie serikali.”

Kufuatia uwepo wa fedha za kushughulikia miradi ya maendeleo, alimtaka Mhandisi Profil Modaha kutimiza wajibu wake na kupata uzowefu kutoka katika Idara ya maji kwa namna wanavyosimamia miradi yao vizuri.

“Mhandisi! hili nililoliona sijalipenda na nitaanza kukuchunguza ili kubaini kuwa kiti hicho ulichokalia kiko sawasawa.”

Akiongea katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya ya Iramba, Suleimana Mwenda alimpongeza meneja wa RUWASA Iramba, Mhandisi Ezra Mwacha kwa namna anavyosimamia miradi ya maji na kubakiza bakaa katika kila mradi anaousimamia.

Aidha, Mwenda alimshukuru Rais Samia kwa kuwajali wananiramba kwa sababu wamepata miradi ya maendelo mingi.

Alisema kuwa ukiachilia mbali miradi ya afya, ICU, jengo la dharura, Vituo vya Afya, zahanati, ujenzi wa shule mpya, madarasa na barabara Iramba imepata mradi wa maji toka ziwa Viktoria Kupitia Shinyanga Tinde wenye gharama ya Tshs 24 bilioni.

Wakiongea na mwandishi wetu kwa nyakati tofauti wananchi wa Iramba na mafundi wamempongeza na kumuombea afya njema Rais Samia ili aendelee kuliongoza Taifa hili na kuendelea kuwakumbuka kuwaletea miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Kapula Kashindi mkazi wa Mwanza alimshukuru Rais Samia kwa miradi hii ya maendeleo kwa sababu imemuwezesha yeye kupata ajira na hivyo kujikuta akiwa Iramba.

“Kwa kweli tunamshukuru sana Rais Samia maana miradi hii ndio imenifanya niwepo hapa kwa sabubu bila miradi hii nisingekuwa hapa.” Alithibitisha

Naye Adamu Kitundu alisema kuwa mwanzoni huduma ya Afya ilikuwa unaipata umbali mrefu hasa kwa akinamama wajawazito pindi wanapokuwa wameshikwa na uchungu lakini kwa sasa kila hatua chache utakuta kutuna kituo cha Afya na hivyo kuokoa uhai wa wananchi.

Ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge ilifika na kukagua ujenzi katika kituo cha Afya Kisiriri kata ya Kisiriri, ujenzi wa jengo la dharura na ICU kata ya Oldi Kiomboi, ujenzi wa Shule mpya na mradi wa maji kata ya Maluga wilayani Iramba.

MWISHO

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.