• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 90 ZIMETUMIKA KUJENGA ZAHANATI YA KIJIJI CHA TUTU ILIYOPO KATA YA KIOMBOI, TARAFA YA KISIRIRI WILAYA YA IRAMBA MKOANI SINGIDA.

Posted on: November 19th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Innocent S Msengi; Amezindua rasmi Zahanati ya Kijiji cha Tutu Kata ya Kiomboi Tarafa ya Kisiriri Wilayani Iramba Zahanati ambayo inakusudiwa kuhudumia wananchi wapatao 1004 katika Kijiji hicho Cha Tutu.


Aidha Msengi, Akiwahutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi, kwa lengo la kushuhudia uzinduzi wa Zahanati hiyo amewataka wananchi hao kuhudhuria kikamilifu na Kupata matibabu katika Zahanati hiyo, kwani kwa sasa changamoto ya kufuata matibabu kwa mwendo mrefu Zahanati ya Bomani umeisha.


Msengi Amesema kuzinduliwa kwa Zahanati hiyo kutaondoa kabisa vifo vya akina Mama na watoto ambao walikuwa wanayapata wakati wanafuata Matibabu Bomani au Hospitali ya Wilaya.


Mwenyekiti huyo wa Halmashauri, Amesema kwa sasa vifo vya akina mama vitapungua kwa asilimia kubwa kutokana na kukamilika kwa Zahanati nyingi katika vijiji Wilayani Iramba, lakini pia pindi vituo vya Afya vya Mtoa, na Shelui vitakapokamilika vitafanya vifo vya mama na mtoto kuwa ni historia katika Wilaya ya Iramba.


Aidha Msengi amebainisha kuwa Mpaka sasa,Tayari Tsh. Bilioni 1.5 zimeletwa kumalizia Zahanati Mbalimbali Huku huduma Katika Kituo Cha Afya Shelui tayari zimeanza, na kuongeza kuwa tayari shilingi Milioni 250 zimeletwa Kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Shati Ili kuhudumia wananchi wa eneo hilo.


Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba Daniel Paul amesema Zahanati ya Tutu imekamilika na tayari imepewa Vifaa tiba huku wahudumu wa Afya tayari amefika kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.


Aidha wananchi wa Kijiji hicho wameishukuru serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali kuhusiana na Afya zao na sasa wamepona kilio chao cha muda mrefu.

"Kituo hiki kimekuja kwenye muda muafaka tunamshukuru sana Rais wetu Mama Samia,Mbunge wetu Mwigulu na Diwani wetu kijana Omary hakika wametufanyia mazuri sana." Amesema Mkazi wa Tutu Noel Mpinga.


Uzinduzi wa huduma Katika Zahanati ya Tutu umefanyika Novemba 19,2024 na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Chama Tawala na Serikali akiwemo Diwani wa Kata ya Kiomboi Omari Hassani Omari, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Jeremia Kahurananga, Afisa Tarafa ya Kisiriri Oswald Leopord, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Iramba na Timu ya uendeshaji wa Hospitali ( CHMT) pamoja na Wananchi wa Kijiji cha Tutu.





Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.