• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ziara ya Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula katika Kijiji cha Nsonga kata ya Kaselya Tarafa ya Ndago kusikiliza kero za wananchi na kuhamasisha maendeleo

Posted on: March 20th, 2019

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, amefanya ziara leo tarehe 20.03.2019 katika kijiji cha Nsonga, kata ya Kaselya Tarafa ya Ndago.

Akiwa katika ziara ya kusikiliza kero za wananchi na kuhamasisha maendeleo, amefika katika Kijiji cha Kaselya, Kata ya Kaselya kutazama shamba la Bwana Salehe Juma aliyepanda miche ya mikorosho 130 hekari nne na nusu iliyotolewa bure na Mhe Rais, John Joseph Magufuli.

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, amempongeza sana na kusema kua Bwana Salehe Juma ni mfano wa kuigwa na kuwataka watendaji wa vijiji kuwasaidia wakulima ili wachungaji wasichungie mifugo katika mimea hiyo.

Naye Salehe Juma amewataka wakulima kuto kukata tamaa, wasiogope, wasubutu kupanda mikorosho kwani mikorosho itakua na watapata soko la korosho.

Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula akikagua shamba la Mhe. Diwani wa Kata ya Kaselya, Charles Dagau aliyepanda Alizeti ya Hyssum 33 iliyohamasishwa na Mhe, Mkuu wa Mkoa, Daktari Rehema Nchimbi.

“Nitoe wito kwa viongozi wengine, Waheshimiwa Madiwani na Watumishi wa Umma wote kuiga mfano wa kilimo hichi kwa kuwa Mhe, Mkuu wa Mkoa, Daktari Rehema Nchimbi anahamasisha tulime Alizeti aina ya hyssum 33 na hii ni alama ya Iramba,” amesema

Akizungumza Mhe, Diwani wa Kata ya Kaselya Tarafa ya Ndago, amehamasika kulima Alizeti hiyo kutokana na uhamasishaji unaofanywa na Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula, kuwataka wananchi walime kwa wingi kilimo cha Alizeti.

“Ninatumia mbolea ya samadi ambayo inauwezo wa kukaa miaka mitatu na ninapokua na mikutano wakati wowote ule ninawahamasisha wananchi wabadilike angalau waachane na mazao yale yanayowapa hasara, natayari wananchi wengi katika kata yangu wanatumia mbegu hii mpya,” amesema

Mhe, Diwani wa Kata ya Kaselya Tarafa ya Ndago amesema, Nimelima hekari 10 za hyssum 33, mahindi hekari 10 na miche ya korosho hekari 10, ninatoa wito kwa jamii katika mazingira yanayokwenda na tekenolojia ya kisasa, tunahitaji kufuata wataalam wanavyotuhamasiha kuwaunga mkono tulime zao la korosho ili litusaidie katika maisha ya baadae.

Akihitimisha ziara yake katika Kata ya Kaselya, Tarafa ya Ndago Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula amewataka viongozi kusimamia miradi ya maendeleo kwa uadilifu na kuhakikisha wafugaji wanawaheshimu wakulima kwa kutoingiza mifugo kuchungia katika mashamba ya Alizeti, Mahindi na Miche ya Mikorosho.

Habari na Hemedi Munga



Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula (wakwanza kulia) akikagua shamba la Mhe, Diwani wa Kata ya Kaselya, Charles Dagau aliyepanda Alizeti ya Hyssum 33 iliyohamasichawa na Mhe, Mkuu wa Mkoa, Daktari Rehema Nchimbi. Picha na Hemedi Munga.


Mhe, Mkuu wa Wilaya, Emmanuel Luhahula (wapili kulia) amefika katika Kijiji cha Kaselya, Kata ya Kaselya kutazama shamba la Bwana Salehe Juma aliyepanda miche ya mikorosho 130 hekari nne na nusu iliyotolewa bure na Mhe Rais, John Joseph Magufuli. Picha na Hemedi Munga.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.