• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ziara ya Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula Kata ya Mbelekese kusikiliza kero na kuhamasisha maendeleo

Posted on: March 22nd, 2019

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amefanya ziara na kufanya mkutano wa hadhara kuongea na wananchi, kusikiliza kero na kuhamasisha shughuli za maendeleo kijiji cha Kikonge, kata ya Mbelekese Tarafa ya Ndago leo tarehe 22.03.2019.

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewataka wananchi kudumisha usafi wa mazingira na kuwataka wazazi kuacha tabia ya kuwalea wanafunzi watoro.

“Niliagiza kila kaya na taasisi zote kujenga choo bora na watendaji wote kukomesha suala la utoro shuleni, endapo atakapopatikana mwanafunzi mtoro kamata mzazi wake ili tuzalishe watoto wasomi na hatutaki kuzalisha wajinga,” amesema

Akiongea Mhe, Mkuu wa Wilaya katika kikao kazi na wataalam mbalimbali amewataka washirikiane vizuri ndipo wataweza kuleta maendeleo kata ya mbelekese.

“Kwenye kata hii hakuna ushirikiano wa watumishi wa umma, ushirikiano ni mdogo, hatuwezi tukaendesha kata kwa kutokua na ushirikiano tudumishe ushirikiano ili tulete maendeleo kata ya Mbelekese,” amesema.

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula amewapa miezi miwili Maafisa Tarafa, na Kaimu Kamanda wa takukuru wilaya, Benjamin Masiyaga kuhakikisha wilaya yote viongozi wanasoma mapato na matumizi na atakaye shindwa kutekeleza atakua hatoshi.

Akiongea katika kikao kazi Shekhe wa Wilaya ya Iramba, Athumani Hussein amemuomba Mhe, Mkuu wa Wilaya kuwahimiza viongozi kusoma mapato na matumizi kwa wananchi ya fedha mbalimbali wanazozikusanya ili kuwajengea Imani ya kufaham fedha iliyochangwa na namna ilivyotumika.

Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula, akiongea na viongozi wa mazehebu mbalimbali ya dini ya kikristu na kiislam kuwashukuru kwa heshima wanayompa Mhe, Mkuu wa Wilaya kwa kuiombea Wilaya ya Iramba iwe salama.

Akiongea na viongozi wa mazehebu katika suala la ulinzi na usalama amewaomba viongozi wa dini kuisadia serikali kuwafichua wale wote wanaotumia makanisa au misikiti kufanya maovu.

“Niwaombe viongozi wa dini mtusaidie kuwa makini kuwafichua watu wanaotumia vyombo vya dini kufanya maovu. Nilazima viongozi wa dini tulinde amani yetu na kudumisha kulinda amani ya wilaya yetu,” amesema

Naye Mhe Diwani wa kata ya Mbelekese amemkabidhi Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Emmanuel Luhahula madawati 146 shule ya sekondari Mbelekese, yanayotokana na juhudi zake za kuhamasisha maendeleo na kukuza ufaulu wa wanafunzi.

Akiongea mbele ya Mkuu wa Wilaya Elizabeth Emmanuel, mwanafunzi wa shule ya Sekondari Mbelekese kidato cha kwanza amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuwakabidhi wanafunzi madawati hayo yanayotatua changamoto walizokua wanazipata na kuwaomba viongozi waendelee na moyo huo huo wa upendo.

Akitoa shukran Mchungaji, Joseph Masensi wa Usharika wa Ndago, amesema wanafurahi sana kwa ushirikiano wanaopatiwa na Mhe, Mkuu wa Wilaya, aidha amemuomba kulitazama upya suala la upatikanaji wa mkaa kwa kua imekua ni changamto kubwa wanaipata kwa sasa.

Habari na Hemedi Munga


Naye Afisa Ardhi, Kennedy Thobias Mpanduji kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, amewakabidhi mwalimu na uongozi wa shule madawati 146 na kuwaomba kuwa na usimamizi mzuri. Aidha amewataka wanafunzi wayatumie vizuri ili baada ya miaka ijayo wadogo zao watakapo kuja wasipate tabu ya madawati na uongozi usichangie tena madawati ispokua wachangie vitu vingine vya maendeleo ya shule ya sekondari Mbelekese. Picha na Hemedi Munga

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.