• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Comments |
Iramba District Council
Iramba District Council

The United Republic of Tanzania Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Iramba District Council

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

DC MWENDA AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI WAPANDA MITI 3500 KATA YA MGONGO

Posted on: March 9th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleimani Yusuph Mwenda ameongoza Wakuu wa divisheni na vitengo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Iramba,Wananchi wilayani hapa kupanda miti 3500 katika  Vijiji vya Kizonzo na Mseko  vilivyopo Kata ya Mgongo ikiwa ni sehemu ya Kampeni ya upandaji miti kwa Wilaya ya Iramba  yenye lengo la kuifanya Iramba iwe ya kijani.

Akizungumzia siku hiyo Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida Suleimani Yusuph Mwenda ,amesema siku ya Upandaji miti imelenga  kuiweka Pamoja Viongozi na Wananchi  ili kushirikiana katika mambo mbalimbali ya kijamii, ambapo aliwataka Wananchi kutoa ushirikiano katika kubaini vitendo vya kihalifu katika jamii.

Aidha, DC Mwenda.  amewataka Wananchi  wa Vijiji hivyo kutunza Miti iliyopandwa  leo Machi 9, 2023 ili ilete tija kwao na kwa kizazi kijacho

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba, Mkuu wa divisheni ya rasilimali watu  amesema kuwa maelekezo ya Kitaifa ni kuhakikisha kila Wilaya inapanda Miti isiyopungua Milioni moja na Laki tano(1,500,000) na kila  Kaya kupanda Miti isiyopungua Minne(4)  ambapo aliwataka Wananchi kutumia jitihada binafsi  katika kufanikisha zoezi hilo.

Afisa  Mtendaji  Kata ya Mgongo ,Maria Daudi  ametaja umuhimu wa zoezi hilo na kueleza mikakati watakayochukua kutunza Miti hiyo ikiwemo kuchukua hatua za kisheria kwa yeyote atakaye bainika kubeza juhudi za Serikali zinazolenga kupambana na mabadiliko ya Tabia Nchi.

Hii ni awamu ya Tatu ya zoezi la upandaji Miti Wilayani hapa ambapo zoezi la kwanza lilianza  siku ya uhuru wa Tanganyika, awamu ya pili ilizinduliwa hivi karibu na Mkuu wa Mkoa wa Singida  na leo ni awamu ya Tatu ambapo jumla ya miti Elfu tatu na mia  tano(3500) Kata ya Mgongo vijiji vya Mseko na Kizonzo

Announcements

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 02, 2026
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • View All

Latest News

  • MAONESHO YA MATUMIZI YA PEMBEJEO ZA KILIMO (MBEGU, MBOLEA NA VIUATILIFU) HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA DISEMBA 29-30, 2025

    December 28, 2025
  • HERI YA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA 2026

    December 25, 2025
  • DC MWENDA AWATAKA WALIMU IRAMBA KUONGEZA UBUNIFU NA BIDII KUINUA UFAULU

    December 09, 2025
  • HERI YA MIAKA 64 YA UHURU WA TANZANIA BARA

    December 09, 2025
  • View All

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
More Videos

Quick Links

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Related Links

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    KIOMBOI, IRAMBA

    Postal Address: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Telephone: 026 - 2532253

    Mobile: 026 - 2533001

    Email: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.