• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Ofisiya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba na Viongozi wa Kata ya Tulya wamefanya ukaguzi wa kushutukiza katika ziwa Kitangiri kata ya Tulya leo 24.09.2018

Posted on: September 24th, 2018

Ofisiya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba na Viongozi wa Kata ya Tulya wamefanya ukaguzi wa kushutukiza katika ziwa Kitangiri kata ya Tulya leo 24.09.2018

Katika ukaguzi huo wamebaini Nyavu haramu nne(4) aina ya  makokoro zenye jumla ya  urefu wa yadi  1900, sawa na futi 5700 na thamani ya Tshs 2,800,000, zimeteketezwa kwa motombele  ya Mkutano wa hadhara wa kijiji najamii ya wavuvi kutoka kijiji cha Doromoni, kata ya Tulya, wilayani Iramba. 

Nyavuhizo haramu zilikamatwa katika Doria iliyofanyika katika ziwa Kitangiri eneo lakambi ya uvuvi  ya Usiulize iliyoko  upande wa Wilaya ya Meatu, ikishirikisha  Kikundi shirikishi cha ulinzi wa ziwa (BMU) Tarehe 19/09/2018 na watuhumiwa kufanikiwa kutoroka na kuterekeza nyavu hizo.

Zoezi hili limefanyika kama utekelezaji wa Sheria ya uvuvi na 22 ya mwaka 2003, Tamko la Mhe. Rais alilolitoa juu  ya kuthibiti matumizi ya makokoro, mpango mkakati wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba kuthibiti matumizi ya zana haramu katika shughuli za uvuvi ziwa kitangiri.

Msimamizi wa sekta ya Uvuvi (W) Ndg. Deogratius K. Isagala, aliongeza kusema Mfumo wa uteketezaji wa makokoro mbele ya mikutano ya hadhara,wananchi  na jamii ya wavuvi mara baada ya wahusika kutoroka na  makokoro yanapokuwa yamekamatwa    ni mkakati wa kutoa somo juu ya kupiga vita matumizi ya Zana haramu za uvuvi wa makokoro katika Ziwa Kitangiri, kuonesha hasara inayoweza kuwapata wavuvi haramu pindi makokoro yanapokuwa yamekamatwa,hivyo kuwa  ni njia ya kisaikolojia yakuwakatisha tamaa wavuvi haramu na njia halisi ya kupunguza idadi ya zana haramu za uvuvi.  Uteketezaji wa nyavu hizo hadharani licha ya kujenga imani miongoni mwa jamii ya wavuvi halali, unathibiti mzunguko haramu wa nyavu haramu zilizokamatwa kurudishwa tena ziwani kwa watendaji wasio waaminifu.

Aidha Baadhi ya athari ya matumizi ya makokoro katika Ziwa Kitangiri ni pamoja na kuvua samaki wadogo wenye ukubwa chini ya inchi 3’ utakaoshusha ubora wa samaki na bei ya soko, uvuvi wa samaki wadogo(parent stock) ambao ni wazazi wa kesho   hivvo kunaweza  kupunguza kiwango cha uzalishaji wa  samaki wa kesho katika ziwa, Kuharibu mayai ya samaki, uvuvi wa makokoro kwa njia ya kuvuta(kukokora)  mara kwa mara kunaharibu sakafu ya ziwa,kuharibu uoto wa asili ndani ya Ziwa na makazi  ya viumbe hai kama vile samaki, wanyama aina ya viboko na mimea iliyomo ndani ya ziwa.

Diwaniwa kata ya Tulya Mhe. Wilfred Kizanga (CCM) amesema Kiwango kidogo cha uzalishaji wa samaki na ubora unawafanya na wavuvi kutumia nguvu na muda mwingi kuvua samaki wachache na wenye bei ndogo ya soko kutokana na matumizi ya muda mrefu ya zana haramu za uvuvi, lakini pale mikakati ya  matumizi ya zana halali itakapofanikiwa na kuzaa matunda  kwa asilimia 100% wavuvi watatumia muda mfupi kuvua samaki wengi wenye ubora na bei nzuri ya soko. 

Aliongeza kusema zoezi hili endelevu limelenga kuhakikisha kuwa Ziwa kitangiri  linaendelea kuwa ni moja ya rasilimali muhimu,iliyopo katika Wilaya ya Iramba, shughuli mbalimbali za uvuvi zinazofanyika katika Ziwa hili zitaendelea kuborekana kutoa mchango mkubwa katika kuboresha lishe ya jamii  na kukuza uchumi wa kipato cha kaya, kuboresha maisha na maendeleo ya wananchi wa Iramba, Igunga,  Kishapu na Meatu na watanzania wote  kwa ujumla na hatimaye kufikia kiwango cha uchumi wa  kati ifikapo mwaka 2025.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • AFISA MWANDIKISHAJI JIMBO LA IRAMBA MAGHARIBI AWATAKA WAENDESHA VIFAA VYA BVR NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • KAMATI YA AFYA YA MSINGI (PHC) IRAMBA YAJADILI MIKAKATI YA CHANJO YA POLIO SINDANO YA PILI

    May 09, 2025
  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.