• Malalamiko |
    • Kuhusu sisi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Maoni |
Iramba District Council
Iramba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Sura
    • Maadili ya Misingi
    • Mikakati
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya kwanza
    • Afya
    • Kilimo
    • Elimu
    • Maji
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Utawala
    • Idara
      • Mipango, Takwimu & Ufuatiliaji
      • Afya
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Idara ya Ardhi na Mipango miji
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Idara ya Mazingira na Usafishaji
      • Elimu Msingi
    • Vitengo
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA NA UHUSIANO
      • Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo Cha Ufugaji Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF
    • Muundo wa Halmashauri
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Riport
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
      • Fomu za Maombi kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Ufugaji
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao Mbalimbali
  • Salary Slip

Mkuu wa wilaya ya iramba mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula amekuatana na kamati ya ushauri ya wilaya ya iramba (DCC) leo tarehe 25 June 2019.

Posted on: June 25th, 2019

Wajumbe wa Kikao cha Ushauri cha wilayani Iramba.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iramba Mhe: Simon Tyosela akichangia maoni yake kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya wilaya ya Iramba.

Mkuu wa wilaya ya iramba mkoani Singida Mhe: Emmanuel Luhahula amekuatana na kamati ya ushauri ya wilaya ya Iramba (DCC) leo tarehe 25 June 2019.

Kikao hicho kimeudhuliwa na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Iramba Mhe: Simon Tyosela, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Iramba Mwl. Linno Mwageni, Waheshimiwa Madiwani na wadau mbalimbali wa maendeleo wa halmashauri ya wilaya ya Iramba.

 

Akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa kikao ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe: Emamanuel Luhahula amesema wadau wote mnakaribishwa kushauri, kukosoa na kuchangia taarifa ya mada kuu ya uanzishwaji wa shamba la serikali kuu la miti ya migunga itoayo gundi katika uwanda wa mbuga ya wembere katika wilaya ya Iramba

Akizungumza na Wadau wa kikao hicho Mhe: Luhahula alisema “Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umejipanga kuanzisha shamba kubwa la mfano kwa nchi nzima la miti ya Gundi kwenye Mkoa wetu ili kuinua uzalishaji wa gundi kwa faida ya jamii na nchi kwa ujumla. Aidha ikumbukwe kuwa Mkoa wa Singida hauna shamba la miti la Serikali Kuu,hii itakuwa ni fursa ya kipekee itakayotoa ajira kwa akina mama na vijana. Shamba hili litarudisha uoto wa asili na viumbe hai waliohatarini kutoweka.

Akitoa ufafanuzi kuhuhu uanzishwaji wa shamba la serikali kuu la miti ya migunga itoayo gundi katika uwanda wa mbuga ya wembere katika wilaya ya Iramba, Meneja Misitu Wilaya Iramba Ndg Shaban J. Nyamasagara lisema “Mbuga ya Wembere katika Mkoa wa Singida ipo katika Wilaya za Iramba na Ikungi. Katika Wilaya ya Iramba vipo jumla ya vijiji 15 vijiji vinavyopitiwa na Mbuga hii ya Wembere ambavyo ni Doromoni Mingela, Nsunsu,  Migilango, Tulya, Luono, Nkonkilangi, Mgongo ,Kisonga-Shelui, Mseko, Msai, Ujungu,Masimba Mlandala na Ndurumo. 

Mbuga hii inaanzia kwenye miinuko ya ardhi nyuzi 06, kusini mashariki ya Mkoa wa Tabora na Kusini Magharibi ya Mkoa wa Singida. Bonde la mbuga hii linaunda maingiliano ya ndani ya maji na Ziwa Eyasi kwa Mkoa wa Arusha. Mbuga ya Wembere imezalisha uoto wa Asili wa nyasi na miti mbali mbali ikiwemo miti aina ya migunga inayozalisha gundi ambayo inakadiriwa kuwa na eneo lipatalo hekta 160,000, ikijumuisha na Wilaya za Igunga, Kishapu na Meatu katika Mikoa ya Jirani ya Tabora,Shinyanga na Simiyu.

Miti inayozalisha gundi kwa wingi ni aina za Migunga ,kitaalamu inajulikana kama Acacia Senegal ambayo huzalisha asilimia 95 ya gundi yote na Acacia seyal,Acacia drepanolobium na aina ziingine kwa asilimia 5. Gundi hii duniani inajulikana kama  ‘dhahabu ya jangwani’.

 

Viumbe wengine katika mbuga ya wembere

Kwa mujibu wa shirika la Kimataifa linalojishughulisha na uhifadhi wa ndege wa porini, ni kuwa mbuga hii ni makao mazuri ya aina tofauti 177 za ndege wa porini. Shirika hili limeainisha aina nne za ndege waliohatarini kutoweka wanaoishi kwenye mbuga hii ambazo  ni,

  •  Agapornis fischeri
  • Histurgops ruficauda
  • Cosmopsarus unicolor na
  •  Francolinus rufopictus.

 

Maana ya gundi

Ni utomvu unaotoka kiasilia kwenye miti ya migunga aina ya Acacia senegal  na aina ziingine za jamii ya migunga hasa wakati wa hali ya ukame na jua kali baada ya mvua kuacha kunyesha, Mti huu utoao gundi (Acacia Senegal)  kwa lugha za wenyeji wa Iramba unaitwa mdulungu ambao hukua kwa urefu wa mita 5- 13

Namna ya kuzalisha miche ya miti ya gundi

Miti hii yaweza kuzalishwa kwa kutumia mbegu. Mbegu hizi zinakuwa salama zikivunwa kabla kasha mbegu (Pod) haijakauka ambapo mbegu husiwa kwenye kitalu kabla ya kupandikizwa kwenye shamba. Aidha unaweza kupanda kwa kutumia pingili kwa baadhi ya miti. Hivyo shamba halisi miche hupandwa kwa nafasi za mita 4 x 4, vilevile kwa kilimo mseto ni mita 10 x 10

Uvunaji wa gundi

Asilimia 95 ya gundi inayotoka kwenye mbuga ya Wembere huvunwa kwenye miti ya migunga inayoitwa  kitaalamu Acacia Senegal na asilimia 5 iliyobaki huvunwa kwenye jamii ziingine za migunga.

Ulinganifu wa uzalishaji gundi duniani

Wazalishaji wakubwa wa Gundi ni Sudani Tani 50,000, Ethiopia Tani 28,000 na Nigeria Tani 17,000 kwa mwaka, wakati huo huo Tanzania tukizalisha tani 1,000 kwa mwaka.

Masoko ya gundi

Gundi ya Tanzania husafirishwa na kuuzwa kwenye nchi za Pakistan, India, Saudi Arabia, Uingereza na Ufaransa pia Makampuni yanayojihusisha na ununuzi wa gundi Tanzania ni pamoja na Mohamed Enterprises, Fida Hussein na Export Trading.

Ushuru wa gundi kwa miaka mitano iliyopita –singida




MWAKA
KILO ZILIZOVUNWA
THAMANI(TSH)
2013
40000
20,000,000
2014
50000
25,000,000
2015
30000
15,000,000
2016
40000
28,000,000
2017
42000
29,400,000
2018
26000
18,200,000
JUMLA

135,600,000

Dhamira ya tfs kuanzisha shamba la miti ya gundi -singida

  • Litakuwa ni  shamba pekee la serikali kuu la miti ya gundi Tanzania.
  1. Kutoa ajira kwa jamii za vijiji jirani na Wilaya kwa ujumla.
  2. Kuongeza chanzo cha mapato kwa jamii, Vijiji, Halmashauri ya Wilaya na Serikali kuu.
  3. Kuvutia utalii wa kuangalia na kupiga picha ndege.
  4. Hifadhi ya mazingira na bioanuai kwa ujumla.
  5. Litahamasisha ufugaji wa nyuki kibiashara kwa jamii.

Faida za gundi kwenye viwanda vya chakula

  • Kusaidia kuhifadhi nyama iliyosagwa kwa muda mrefu na kuifanya ivutike.
  1. Kutunza ladha kwenye vinywaji.
  2. Kuunganisha unga unaotengenezewa sukari na kutoa umbo linalotakiwa.
  3. Husaidia kutengeneza povu la kiwango kinachotakiwa pamoja na rangi kwenye bia na mvinyo.

Faida za gundi kwenye madawa

  • Hutibu kutokwa damu kwenye fizi.
  1. Huondoa sumu mwilini, mafuta mabaya na mchafuko wa tumbo.
  2. Hutumika kwenye dawa za kupunguza uzito.
  3. Hutumika kutengeneza Viberiti, vifaa vya udongo, rangi za maji, Vidonge, Wino wa komputa, marashi, viuadudu n.k.

Matumizi ya wenyeji.

  • Mbegu zake ni chakula cha binadamu.
  1. Huongeza rutuba ya udongo.
  2. Hutengenezewa kamba kwa matumizi ya nyumbani.
  3. Majani pamoja na kasha mbegu ni chakula cha mifugo.
  4. Maua hutoa chamvua kwa nyuki.Asali yake ina ubora mzuri.

Vikwazo vya uzalishaji gundi

  • Ufyekaji wa miti ya gundi kwa ajili ya kilimo na makazi.
  1. Nzige waharibifu wa majani ya miti.
  2. Panya wanaokula gundi.
  3. Upungufu wa madini ya chumvi kwa miti ya gundi hasa mvua zinapozidi.

Tangazo

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI June 05, 2025
  • ZOEZI LA CHANJO YA KITAIFA YA HOMA YA MAPAFU KWA NG'OMBE, SOTOKA KWA MBUZI NA KONDOO, NA MDONDO KWA KUKU January 08, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO YA 10% INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KWA ROBO YA PILI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025. March 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI IRAMBA October 02, 2024
  • Angalia Zaidi

Habari mpya

  • DC MWENDA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA AMALI KITUKUTU

    May 08, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YA HALMASHAURI YA WILAYA YA IRAMBA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

    May 06, 2025
  • DC MWENDA ATOA WITO KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI KUIMARISHA UFUNDISHAJI KWA MADARASA YA MITIHANI

    May 06, 2025
  • JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI WILAYANI IRAMBA LATOA ELIMU YA KINGA DHIDI MAJANGA YA MOTO KWA MADIWANI NA WANANCHI

    May 02, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

wanafunzi wakiimba wimbo wa TAZAMA RAMANI katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wilayani Iramba
Video Zaidi

Linki za Haraka

  • Organisation Structure
  • Mission and Vision
  • Reports
  • Water Department

Linki Zinazohusiana

  • OFISI YA RAIS-TAMISEMI
  • OFISI YA RAIS-UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • WATUMISHI PORTAL
  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
  • SEKRETARIETI YA AJIRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Kuhusu sisi

    KIOMBOI, IRAMBA

    Anuani ya Posta: P.O BOX 155. KIOMBOI-IRAMBA

    Simu: 026 - 2532253

    Simu: 026 - 2533001

    Barua pepe: ded.irambadc@singida.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • FAQ
    • Sitemap
    • Huduma

Copyright ©2017 Iramba District Council . All rights reserved.